Monday, 15 February 2016
Saturday, 7 February 2015
KATIBA MPYA, MGOMBEA HURU KUKUZA DEMOKRASIA TANZANIA

NA JACKLINE MAJURE ( WAKILI MAHAKAMA
KUU)
Ibara ya 216.-(1) katika rasimu inayopendekezwa ili iwe
katiba kama itapita inasema kama
ifuatavyo “Bila kuathiri masharti ya Ibara ya 88
na Ibara ya 140, mtu atakuwa na haki ya kuwa mgombea huru katika uchaguzi
unaosimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi”.
Ni kwa maana hii kuwa ule
utaratibu wetu wa kuwa
kila mgombea ubunge au urais au udiwani
ni lazima awe ametokana na chama chochote cha siasa
utakuwa umekufa. Haufi kwa maana
kuwa vyama sasa vimepigwa marufuku
hapana, isipokuwa si lazima kupitia chama cha siasa ili mtu awe
kiongozi kwa njia ya
kuchaguliwa.
Mgombea huru atakuwa ni mgombea ambaye hatokani na chama chochote
cha siasa na ataweza kugombea
ubunge udiwani na hata mamlaka
makubwa ya urais ataruhusiwa kugombea. Pia ugombea huru umeainishwa kama
sifa maalum kwa mtu ambaye havutiwi na siasa za vyama katika kugombea ubunge.
Ibara ya 140( 1 ) inasema hivi
“Bila kuathiri masharti yaliyomo
katika Ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa
mbunge endapo:
|
(a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano
aliyetimiza umri wa miaka ishirini na moja wakati wa kugombea;
|
(b) anajua kusoma na
kuandika lugha ya Kiswahili au Kingereza; na
|
(c) ni mwanachama
aliyependekezwa na chama cha siasa au mgombea HURU.
|
Baada ya kutimiza sifa zilizoainishwa ambazo ni kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano, kujua kusoma
na kuandika kati ya lugha ya
Kiswahili ama kiingereza lakini basi mtu asiye
na chama chochote cha siasa anaweza
kuomba ridhaa ya wananchi ili awe mwakilishi wao bungeni. Kwa mamlaka ya rais Ibara ya 88 baada ya sifa nyingine kutimia imetoa ruksa
kwa mgombea huru kuwania mamlaka
hayo kama ifuatavyo ;
88.-(1)
Mtu atakuwa na sifa ya kuchaguliwa kushika nafasi ya madaraka ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano ikiwa:
|
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya
Muungano
|
(f) ni mwanachama na
mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa au mgombea HURU.
|
Aidha katika yote hayo ibara ya 143.-(1) inaibua kitu kingine
kuhusu mgombea binafsi kama inavyonukuliwa hapa, “Mbunge atakoma kuwa Mbunge ikiwa
litatokea lolote kati ya mambo yafuatayo:
(h) Mbunge aliyetokana na mgombea huru,
atajiunga na chama chochote cha siasa”
|
Kawaida tumezoea kusikia diwani,mbunge au rais akiacha chama
chake cha siasa anapoteza hata mamlaka yake. Ni kwasababu hii tumeshashuhudia
mara nyingi baadhi ya viongozi wa siasa wakikimbilia
mahakamani kulinda nyadhifa zao baada ya
kutishiwa uanachama wao kwenye
vyama vyao vya siasa. Kwahiyo kama zamani kuacha uanachama ilikuwa ndio upoteze mamlaka
sasa hata kuingia uanachama nako
kutampelekea mwanasiasa kupoteza mamlaka. Kwa ufupi tuangalie faida na hasara za mgombea huru katika
ibara hizi.
FAIDA ZA MGOMBEA
HURU
( a ) Kwanza imepanua wigo wa
demokrasia kwa kuwashrikisha watu wengi zaidi katika kuomba ridhaa ya nyadhifa mbambnali. Wako watu wengi ambao walikuwa
wakitaka nyadhifa za siasa lakini
hawapendi siasa za vyama. Kwa
ibara hii ni kusema kuwa hawa nao
wameingizwa katika kinyanganyiro na
hivyo sasa ushiriki utaongezeka.
( b ) Mgombea binafsi atongeza ushindani hasa majimboni. Wako watu ambao walikuwa na
uwezo mzuri wa kuwa viongozi na wanakubalika sana kwa
wananchi lakini wanaenguliwa katika kinyanganyiro kutokana na hila ndani ya vyama. Kwa kuwapo
mgombea huru itakuwa
chama kikimuengua mtu anayekubalika
kwa wananchi basi kijiandae kupambana naye kwa ushindani mkubwa katika uchaguzi.
( c )Itapelekea kupatikana viongozi wenye uwezo kiuongozi na si kiongozi mwenye uwezo kimtandao wa siasa. Mara nyingi viongozi wanaopatikana
kupitia vyama vya siasa ni wale wenye
mitandao madhubuti katika vyama hivyo
na si wale wenye uwezo kuiongozi.
Hili wala sio siri viongozi wetu wengi wamepatikana kwa nguvu za mitandao hasa
mitandao fedha na si uwezo binafsi
kiuongozi
0784482959, 0714047241
WAKULIMA, WAFUGAJI,WAVUVI NI HAKI SASA KUISHITAKI SERIKALI WASIPOTENGEWA MAENEO MAALUM, KATIBA MPYA

NA
EMMANUEL MARWA ( WAKILI
MAHAKAMA KUU).
Rasimu inayopendekezwa ili
iwe katiba inayo mambo mengi mapya.
Ni sahihi kusema mapya
kwakuwa ni mambo ambayo hayapo
katika katiba yetu tuliyonayo sasa. Moja ya mambo hayo ni hili la kuingiza au kuweka haki za
wafugaji na wakulima, wachimbaji na wavuvi. Haya ni
makundi muhimu sana katika jamii yetu
hasa kutokana na ukweli kuwa mpaka sasa kundi
kama la wakulima ndilo linaloonekana
kubeba asilimia kubwa ya watu wote katika nchi hii.
Kwa ukweli kama huu kupata
katiba au sheria ambamo haki na
mustakabali wa watu kama hawa
unatajwa si jambo la kubeza.
( a ) MALALAMIKO YA MAKUNDI YA
WAKULIMA, WAFUGAJI, WAVUVI, WACHIMBA
MADINI.
Kwa muda mrefu
sasa kumekuwepo na malalamiko
kutoka kwa makundi hasa ya
wakulima , wafugaji na
wachimba madini. Malalamiko yao makubwa wamekuwa wakiyaelekeza kwa serikali na kubwa zaidi wakiilalamikia serikali kutokuwa na sera maalum ya
kuwatengea maeneo ya kulima, malisho, kuvua pamoja
na maeneo ya kuchimba madini.
Hali hii haikuwa imeishia katika malalamiko tu bali
ilishapiga hatua na kuwa
mgogoro mkubwa ambao sasa ulikuwa
unaelekea kuwa janga la kitaifa. Na hali ilikuwa inakuwa mbaya zaidi pale makundi haya yanapoanza kugombea maeneo kwa mfano
tumeshuhudia mara kwa mara tena
katika maeneo mbalimbali ya nchi kundi la wakulima na kundi la wafugaji wakigombea maeneo.
Hali ilikuwa tete hasa
pale ilipokuwa ikiripotiwa vifo na majeruhi kutokana na magomvi
hayo. Tatizo kubwa ilikuwa ni kukosekana
kwa hiki ambacho sasa kinaelezwa
na rasimu hapa chini.
( b ) WAKULIMA, WAFUGAJI, WAVUVI,
WACHIMBA MADINI KUTENGEWA MAENEO YAO
RASMI.
Ibara ya 46 ( 2 ) inasema kuwa Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa
kisheria kwa madhumuni ya kubainisha na kutenga maeneo ya ardhi kwa ajili ya
matumizi ya kundi la Wakulima, wafugaji, wavuvi na wachimbaji madini.
Ibara kama hii ni ibara muhimu
kwa mustakabali wa uchumi na
amani ya nchi yetu.Makundi ya jamii
hizi ni makundi ambayo yamekuwa yakiongezeka kwa kasi ya ajabu.
Hatari
kubwa ambayo imekuwa ikitukabili kama
taifa ni kuwa wakati makundi ya
wakulima, wafugaji na wavuvi yakiongezeka
kwa haraka mno ardhi tuliyonayo
imekuwa ikibaki ileile. Hii ni kusema kuwa mahitaji ya ardhi yanaongezeka
wakati ardhi haiongezeki. Kwa usemi huu
kila mtu anaweza akapima hatari ambayo kama taifa tulikuwa tunaanza
kukabiliana nayo.
Ni bomu kubwa lililokuwa likijitega taratibu. Kutokana na hali kuwa
hivi ilikuwa basi
inahitajika sera madhubuti ya kudhibiti hali hii. Na sera ya kudhibiti hali kama hii haikupaswa kuwa sera ya kawaida. Ilitakiwa kuwa sera inayotokana na sheria kuu kama katiba. Na hiki
ndicho kilichofanyika.Pamoja na
hayo zipo haki nyingine za makundi haya kama
tutakavyoona hapa chini.
( c ) SASA NI LAZIMA WAKULIMA, WAFUGAJI KUPEWA TAARIFA KUHUSU
SHUGHULI ZAO.
Ibara
hiyohiyo ya 46 (b) inazidi kusema kuwa wakulima.wafugaj,wavuvi na wachimba
madini watakuwa na haki ya kupata
taarifa na maarifa kwa lengo la kuboresha kilimo, ufugaji, uvuvi na uchimbaji
madini.Hapo juu tumeona haki ya makundi
haya kutengewa maeneo maalum. Hapa sasa tunaona haki yao ya kupata taarifa ikiwa ni pamoja na maarifa.
Taarifa
maana yake ni kuwa serikali sasa
inalazimika kuweka mitandao ya kuwapasha
habari wakulima, wafugaji na wachimba madini kuhusu shughuli zao. Kwa hiyo kuwapasha
habari si hiyari tena isipokuwa lazima
maana ni takwa la kikatiba.
Kwa
upande wa maarifa ni kama kuwaaandalia
semina, majukwaa ya mijadala ya
kielimu,kuwaunganisha na shule za
kilimo,mifugo na uvuvi, vipeperushi na vijarida na kuwaandaa kwa kila kitu
kuhusu elimu. Hili nalo si la hiyari tena kwakuwa litakuwa kikatiba.
( d ) WAKULIMA, WAFUGAJI, WACHIMBA MADINI NA
HAKI YA KUMILIKI
ARDHI.
Ibara
hiyohiyo ya 46 ( a ) inawapa tena
wakulima, wafugaji,wavuvi, wachimba madini haki ya kumiliki ardhi kwa kusema kuwa (a) wakulima, wafugaji,wavuvi,
wachimba madini watakuwa na haki ya kumiliki, kutumia na kuendeleza ardhi kwa
ajili ya shughuli zao;
Kama Watanzania wengine
haki ya kutumia na kumiliki ardhi walikuwa nayo hata kabla ya rasimu hii.
Lakini sasa kuiweka katika Katiba na huku ikiwarejea wao peke yao ni jambo la mafanikio na linaloonesha
ni kwa namna gani ipo ari
ya kushughulikia matatizo yao. Pia inaonesha ni kwa kiasi gani makundi haya sasa yanatambulika rasmi na haki zao zinatofautishwa na haki za makundi mengine.
( e ) UMUHIMU AU
FAIDA KATIKA IBARA HIZI JUU.
Kuna kitu kikubwa kimoja ambacho kinajitokeza na kuwa kama faida kubwa ya ibara nilizoeleza hapa juu. Kutokana na ibara kuwa
katika mtindo huo tuliouona hapo juu
sasa ieleweke wazi kuwa makundi yote yaliyotajwa katika ibara hizi
yamepata ruhusa ya kuifungulia
mashtaka serikali iwapo lolote katika yaliyoorodheshwa kama haki zao hayakutekelezwa.
Hii ina maana baada ya
kupita kwa rasimu na kuwa katiba
wakulima, wavuvi, wachimba madini wasipotengewa maeneo maalum kwa ajili ya shughuli
zao basi
wanaweza kuishtaki serikali kwa
maombi maalum( petition) na wakapata
haki hizo ikiwemo fidia. Kwa hiyo sasa ni kusema kwamba suala la
serikali kutenga maeneo maalum kwa ajili ya makundi
haya sasa ni la
lazima.
0784482959, 0714047241
KATIBA MPYA, KIGEZO CHA SHAHADA KWA MGOMBEA URAIS SASA KUTUPATIA RAIS BORA .
Ni siku muhimu tena katika
uchambuzi wa Ibara mbalimbali katika rasimu inayopendekezwa ili ikipita iwe
katiba. Upo umuhimu mkubwa sana kwa Watanzania kujua kilichomo ndani
ya rasimu hii kwakuwa leo hii inaitwa rasimu lakini kesho itaitwa
sheria na kila mtu anayejua kilichomo na
asiyejua wote watalazimika kuwajibika kwake bila kukiuka .
Kwa msingi huu elimu na
hamasa zaidi inahitajika ili kumfanya kila
mtu aone hili linamhusu kabla ya kuanza kulalamika kwa kuonewa
itakapoanza kutekelezwa kwa lazima. Katika mwendelezo wa uchambuzi wa Ibara
zilizomo katika rasimu leo tujikite
katika Sura ya Nane Sehemu ya Kwanza (
b ) Ibara ya 85 ( 1 ) ( e ) ambayo inanukuliwa hivi
“Mtu
atakuwa na sifa ya kuchaguliwa kushika nafasi
ya madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ikiwa anayo shahada ya chuo cha
elimu ya juu kinachotambuliwa kwa
mujibu
wa sheria, au awe na ujuzi na uzoefu wa uongozi katika
ngazi
ya taifa utakaomwezesha kumudu madaraka ya Rais”
Ibara
ya namna hii ni mara ya kwanza kabisa
katika historia ya nchi yetu kuingia katika
katiba. Pamoja na mabadiliko mengi yaliyowahi kufanyika kwenye katiba kigezo hiki
hakikuwahi kuingizwa.
Siwezi
kusema waliopendekeza ibara hii kuwemo walilenga nini lakini kwa akili ya kawaida kabisa utaona kuwa wamezingatia zaidi mabadiliko
makubwa ya kidunia. Hapo awali sifa ya
kuwa mgombea urais ilikuwa uwezo wa kujua na kusoma na kuandika. Aliyejua
kusoma na kuandika na sifa nyingine ilimtosha kuizuru tume tayari kwa kuchukua
fomu ya nafasi ya rais.
Leo
rasimu ikipita ina maana hata mwenye stashahada(diploma) haruhusiwi
kuusogolea urais.
Aidha
ukiisoma vizuri ibara utaona kuwa hata stashahada ya juu ( Advanced diploma)
ambayo kwa mwenendo wetu wa elimu
imekuwa ikichukuliwa kuwa na hadhi sawa
na shahada(degree) imekataliwa katika kuukwaa urais.
Kitu
kingine ambacho kimejitokeza katika ibara hiyo ni pale inapoainishwa sifa nyingine ambayo ni ujuzi na uzoefu wa uongozi katika ngazi ya taifa utakaomwezesha kumudu madaraka ya rais. Ibara imekaa hivi, kwanza awe na shahada ya kwanza kutoka chuo kinachotambulika au
awe na uzoefu na ujuzi katika uongozi ngazi ya taifa wa kumwezesha kumudu
madaraka ya rais.
Nimekariri
hilo neno “au” hapo juu kwakuwa lina maana kubwa katika ibara hii. Maana ya neno au ni kuwa anayeutaka urais awe na kimoja kati ya elimu ya shahada au uzoefu.
Hii maana yake ni kuwa inawezekana ukawa hata na elimu ya darasa la saba lakini ikiwa unao uzoefu katika uongozi wa taifa basi umepata sifa
kikatiba ya kugombea.
Ingekuwa
imesema awe na shahada pamoja na
uzoefu basi ingekuwa maana yake
vinatakiwa vyote viwili lakini kumbe
hata kimoja tu elimu au uzoefu
inakuwa tayari ni sifa kwa mujibu
wa ibara hii. Ufafanuzi wetu hapa huwa ni ufafanuzi wenye uwiano(balanced
description). Huwa inaelezwa ibara kama
tulivyoona hapo juu halafu zinaelezwa faida zake na hasara zake ili iwe nafasi
kwa msomaji mwenyewe kwa kutumia akili kuona lipi jema kwa mustakabali wa leo
na kesho katika taifa na lipi si jema.Hivyo basi hapa chini zinaelezwa faida na
hasara za Ibara hii.
FAIDA
AU UZURI WA IBARA
HII.
( a ) Kwanza kabisa kwa kuweka kigezo cha elimu ya kiwango cha juu kama shahada ibara hii
imezingatia sana hatua kubwa ambayo dunia imepiga. Ukweli ni kuwa
uendeshaji wa nchi wa sasa ni uendeshaji
unaohitaji uelewa mkubwa unaotokana
pamoja na mambo mengine na kiwango kikubwa cha elimu kama shahada.
Yapo
mambo makubwa ya kitaalam yanahitaji
ukokotozi na uelewa wa hali ya juu kwa mfano
mambo ya miamala ya kodi, sheria za kimataifa, mikataba mikubwa,
upangaji wa sera makini, uwezo wa
kutafiti na kuendana na mabadiliko
makubwa ya kiteknolojia n.k.
Hayo
yote yanahitaji shule kubwa kwa hili wala tusiongee sana. Ni kweli rais anakuwa na wasaidizi wake ambao
kimsingi ndio wataalam haswa. Lakini hilo haliondoa ulazima wa yeye kutakiwa
kujua mambo hayo pia. Hii ni kwakuwa pamoja na mambo kufanywa na wasaidizi
mwisho wa siku lazima naye apitie na atoe ushauri, amri au maagizo kuhusiana
nayo. Atawezaje kutoa maagizo kwenye mikataba mikubwa ya kiamataifa au jambo
kubwa linalohusu sera za nchi bila kuwa na
elimu kubwa.
Atashauri
nini kama hajui. Si atakuwa wa kudanganywa na watendaji na mwisho wa siku taifa
linaangamia. Huo ni ukweli mtupu na
hakuna namna ya kuusema isipokuwa hivihivi ulivyosemwa. Kwa ufupi twaweza kusema kuwa kwa ibara hii
tutampata rais mweledi( professionalism)
na huu ndo utakuwa uzuri wa kwanza wa ibara hii.
( b )Faida au uzuri mwingine wa ibara hii ni kuwa kwa kusema kuwa mtu awe na shahada au ujuzi na uzoefu katika uongozi ibara
imejitahidi kuwaingiza watu wengine
ambao hawatakuwa na shahada lakini wamekuwa katika uongozi kwa ngazi ya taifa kwa
muda mrefu, wamekuwa waadilifu na wanao ujuzi wa kutosha wa kuwawezesha kushika kiti cha rais.
Ni
ukweli kuwa kuwa ndani ya serikali wamo watu wengi ambao hawana hizi shahada
lakini wamekuwa katika uongozi wa taifa kwa muda mrefu na wanao ujuzi wa kuongoza pengine kuliko
hata hao wenye shahada zao. Tunao wanasiasa wengi wakongwe ambao wengi wao kutokana na kusoma zamani
au vinginevyo hawana
shahada lakini ni wazuri sana katika
uongozi. Wapo wengine waliwahi kuwa mawaziri huko nyuma, makatibu wakuu,
wabunge na nyadhifa nyingine nyingi. Hawa nao wamepewa nafasi na ibara hii kwa
sifa yao ya ujuzi na uzoefu.
0784482959
0714047241
TUJIHADHARI NA MATUMIZI YA DEMOKRASIA, KATIBA MPYA
Sura ya pili, sehemu ya pili ibara ya 12( 1 ) ya rasimu inayopendekezwa
kuwa katiba inasema kuwa
“Lengo
la Katiba hii kisiasa ni kudumisha demokrasia”.
Rasimu inayasema haya ikiwa katika
harakati za kuelezea malengo ya taifa ya kisiasa.Kimsingi katika rasimu yako malengo ya taifa ya kijamii(
social vision), malengo ya taifa ya kiutamaduni( cultural vision), malengo ya
taifa ya kiuchumi( economic vision) na malengo ya taifa kisiasa( political vision) ambayo ndio tunayaangalia
sasa.
Ukisikia malengo ya taifa kisiasa au
kijamii maana yake ni mwelekeo wa
taifa kisiasa au kijamii. Mwelekeo maana
yake ni kuwa kila kitakachokuwa
kinafanyika nchini lazima kiwe kinafanana na kile kilichosemwa katika katiba. Taasisi zote za dola na za kiraia lazima
zihakikishe shughuli zake zote zinafanana na lengo la kisiasa katika katiba. Na
kwakuwa lengo la kisiasa ni demokrasia basi
kila taasisi ya kidola au binafsi lazima ihakikishe shughuli zake zinafanana na demokrasia.
Hii maana yake ni kuwa demokrasia itakuwa ndio kioo. Taasisi au mtu
binafsi atakuwa anatakiwa kujitazama na
kuona kama anafanana na demokrasia
iliyosemwa katika katiba ambapo akiona anafanana basi hiyo shughuli anayoifanya ni halali kwakuwa ina baraka za katiba na akiona haifanani
basi shughuli hiyo ni haramu na yuko katika hatari ya kuchukuliwa hatua za
kisheria kwa kukiuka katiba.
Ni sawa na kusema kuwa demokrasia kiwe ndio kiigizo chetu, iwe
ndio mfano wetu.Hiyo ndio maana ya demokrasia kuwa lengo la taifa kisiasa. Kwa
maneno kama haya utaona ni kwa namna gani demokrasia imetukuzwa na kupewa hashima ya pekee kiasi cha
kupendekezwa kuwa kiigizo kwa Watanzania zaidi ya milioni 45.
Hii demokrasia nini mpaka ipate heshima kubwa
kiasi cha kuwa lengo kuu,kiigizo kikuu, mwelekeo mkuu,
na mfano mkuu wa watu zaidi ya milioni
45 kitaifa.
DEMOKRASIA NININI.
Ziko tafsiri nyingi na maarufu za
demokrasia ambazo wengi wetu tunazijua.
Sitaeleza tafsiri yoyote katika hizo isipokuwa nitaeleza wazo la jumla kuhusu hiki
kitu kinachoitwa demokrasia ambacho
katiba yetu mpya imetuelekeza
kukisujudia.
Ukitaka kumweleza mtu wa kawaida kabisa maana ya demokrasia mwambie hivi, demokrasia ni
haya maisha unayoyaona sasa,watu wanavaa wanavyotaka, watu wanatembea kulala na
kula wanavyotaka, mtu anaamua awanie uongozi au hapana, mtu anaamua nani awe kiongozi wake na nani asiwe, mtu
anaoa au kuolewa na anayemtaka, mtu anamkosoa
anayemtaka awe kiongozi wake mkuu au
mdogo, mtu anazungumza anavyotaka , mtu anaruhusiwa kuishi popote na bila kubughudhiwa,
yaani kwa ufupi kila uhuru wa kutenda
jambo unaouona hiyo ndio demokrasia.Mtu atakuelewa vyema.
DEMOKRASIA NDIO UBEPARI
Matendo ya kufanya mambo kwa uhuru
yameanza mamilioni ya miaka iliyopita isipokuwa hayakuwa yakiitwa demokrasia.
Walioanzisha demokrasia walichukua baadhi ya
matendo huru wakayaingiza katika huo mfumo wao wakayaita demokrasia.
Lakini
matendo kama uhuru wa kuongea(maoni), kutembea , kuvaa n.k yalikuwapo kabla ya
kitu kiitwacho demokrasia na umri wa matendo haya waweza kuwa sawa na umri wa
mwanadamu duniani.Aidha demokrasia hii tuliyonayo leo imeanza karne ya 15 kipindi cha hatua ya kwanza ya ubepari(
mechantalism) na imekua mpaka hatua ya sasa ya ubepari ambayo huitwa ubepari uliokomaa(monopoly
capitalism).
Kimsingi demokrasia ndio sera kuu ya
ubepari na neno demokrasia limeanzishwa na mabepari. Kwa maana hiyo tunapoamrishwa na katiba kuwa
demokrasia iwe ndio kiigizo, chetu, na
mfano wetu tunaambiwa kuwa kiigizo, na mfano wetu uwe ubepari.Ubepari(Capitalism)
ndio unaomiliki kitu kiitwacho demokrasia hili wala halina shaka. Kwa ibara hii
maana yake ni kuwa mwelekeo wa nchi hii ni ubepari na nchi hii sasa ni ya
kibepari rasmi.
MATATIZO YA KUFUATA UBEPARI.
( a )
Ielewewke kwamba ubepari ni mali ya watu na bila shaka walioanzisha na kumiliki
mali hiyo wanayo malengo yao. Miaka ya nyuma kiongozi wa ubepari alikuwa Wingereza
na sasa kiongozi wa ubepari ni Marekani. Wakati Wingereza akiongoza ubepari
alitumia nafasi hiyo hasa kwa mgongo wa
demokrasia kuingia Afrika na kuitawala
Afrika akishirikiana na wenzake wa ulaya.
Walijifanya wamekuja na mfumo mpya wa uongozi ambao ungeweza kumaliza
matatizo na shida za watu huku wakijua
na kuamini kuwa mfumo huo wenyeji wasingeweza
kumudu misingi yake kutokana na elimu na weledi mdogo na hivyo kujikuta
wameangukia mikononi mwa wageni.Kwa ufupi tuliweza kutawaliwa kwa urahisi
kutokana na kuzidiwa na mbinu za hiki kinachoitwa demokrasia.
( b )
Leo Amerika ameweza kuwa na amri juu ya dunia kupitia hiki kitu kinachoitwa
demokrasia. Mila na tamaduni za asili ambazo zimezaa maadili mema na mwenendo
mwema katika jamii zetu kwa muda mrefu zimekufa
na zimeuliwa na hiki kiumbe demokrasia.Tunashuhudia mavazi ya
hovyo,vitendo vya ukahaba, ushoga,
heshima kutoweka kwa mkubwa na mdogo, usagaji, na ghasia nyingine nyingi kwa
mgongo wa huyu demokrasia.
( c )
Wameandaa vitu wakaviita misingi mikuu ya demokrasia huku wakiamini kuwa hakuna
yeyote atakayeweza kufaidika na vitu
hivyo isipokuwa wao. Mfano, moja ya msingi wa demokrasia ni kuwa na uhuru
katika uchumi au uchumi huria. Katika uchumi huru ndimo penye uwekezaji kimataifa.
Ndani ya uwekezaji wa kimataifa
ndimo ilimo fursa ya wao kuja kuogelea
katika rasilimali zetu. Walijua uhuru katika uwekezaji wa kimataifa hakuna mwafrika atayekuwa
na uwezo wa kuwekeza kitu cha maana kwao. Isipokuwa wao ndio wataokuja
kuvinjari ndani ya migodi yetu,maziwa yetu, bahari, mafuta, gesi, na kila kitu.Demokrasia
ni mali ya watu na wenye nayo wanayo malengo
yao.
Tunatoa uhauri kuwa pamoja na maono
mazuri ya katibas mpya katika kukuza na kuimarisha
demokrasia tunapenda kusema
kama alivyosema aliyekuwa
rais wa Libya marehemu Kanali Muammar Gaddafi kuwa demokrasia nzuri
ni ile isiyoharibu mila desturi za wenyeji pia ni
ile isiyotumka kuingiza fikra za
kinyonyaji.
0784482959
0714047241
KINGA DHIDI YA MASHTAKA YA RAIS KUMFANYA RAIS AJAYE KUJIAMINI KUSHUGHULIKIA UFISADI.
NA
JACKLINE MAJURE (WAKILI
MAHAKAMA KUU)
Ibara ya 93 katika rasimu
inayopendekezwa ili iwe katiba inasema
hivi 93.-(1)”
Wakati Rais akiwa madarakani, hatashtakiwa wala mtu yeyote
hataendesha
mashtaka ya aina yoyote dhidi yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la
jinai”.
Ni
aina ya ibara ambayo inatoa kinga kwa mtu atakayekuwa ameshika madaraka ya rais kutoshitakiwa. Katika ibara hii
kuna mambo matatu ya kuzingatia, Kwanza
kabisa ibara hii inazungumzia wakati
rais anapokuwa madarakani yaani wakati yuko
ikulu ndo asifunguliwe mashtaka, lakini
pili mashtaka yenyewe ambayo hapaswi kufunguliwa ni yale Mashtaka ya kijinai tu ambayo ni kama kuua,
kubaka, kulawiti,kupiga, kuiba, rushwa, uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya
ofisi n.k. Tatu sehemu anapozuiwa kushtakiwa ni mahakamani wala si bungeni.
Kwa
kawaida viongozi wakuu hasa marais wakati mwingine hushtakiwa mahakamani au
bungeni lakini kwa hapa imezuiwa
kumshtaki makahamani wala si bungeni.Kwahiyo ibara hii ndogo ya ( 1 ) imeundwa
na mambo hayo matatu.
Aidha Ibara hiyohiyo Ibara
ndogo ya (2) inasema hivi
“Wakati Rais ameshika madaraka kwa mujibu wa Katiba hii,haitaruhusiwa
kufungua mahakamani shauri la madai kuhusu jambo lolote alilolitenda au
alilokosa kulitenda yeye binafsi kama Rais ama kabla au baada ya kushika
madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku thelathini kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais atapewa au
ametumiwa taarifa ya madai kwa maandishi
kwa kufuata utaratibu utakaowekwa kwa mujibu wa sheria, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo kuhusu chanzo cha
shauri hilo, kiini cha madai yenyewe,
jina lake na anwani ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai”
Ibara
hii inatoa nafasi kwa rais aliye madarakani kushtakiwa kwa makosa ya madai. Ile
ibara ya kwanza ya juu inakataza kumshtraki kwa makosa ya jinai wakati akiwa
madarakani. Hii sasa inaruhusu kushtakiwa hata akiwa madarakani lakini kwa
makosa ya madai tu. Makosa ya madai ni kama kugombea mashamba,viwanja au
nyumba, kukopeshana vitu vya thamani kama fedha na kushindwa kulipa, kudai
fidia baada ya kutukanwa au kudhalilishwa,kuvunja mkataba kama mikataba ya
mauziano ya vitu kama magari n.k. Hayo ndio makosa ya madai ambayo rais hata akiwa madarakani
waweza kumshtaki nayo.
Aidha jambo jingine la
tofauti limejitokeza katka ibara
hiyohiyo ya 93 ibara ndogo ya (3) ambayo inasema hivi “ Isipokuwa kama ataacha kushika
madaraka ya Rais kutokana na kuondolewa madarakani na Bunge, haitakuwa halali
kwa mtu kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la madai dhidi
ya mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo
kutokana na jambo
alilofanya
wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais”.
Kwanza tuliona hairuhisiwi kumshtaki
rais kwa kosa lolote la jinai pale anapokua madarakani, pili tumeona
inaruhusiwa kumshtaki rais kwa kosa la madai hata akiwa madarakani na sasa
tunaona kuwa itakapotokea bunge limemwondoa rais madarakani basi hakuna ruhusa mtu au chombo chochote kumshtaki rais kwa kosa
lolote liwe la jinai au la madai alilofanya akiwa madarakani.
Sura ya jumla ya ibara hizi zote kwa pamoja ni
kuwa kwanza rais hashtakiwi kwa kosa lolote la jinai iwe pale anapokuwa madarakani au hata baada
ya kutoka. Makosa yote ya jinai aliyoyafanya wakati akiwa ikulu hayaguswi
kabisa. Pili ni kuwa anayetaka kumshtaki
rais kwa kosa la madai amshtaki akiwa bado yuko madarakani lakini akishatoka
basi huwezi tena kumshtaki hasa kama ametoka kwa kuondolewa na bunge. Tuangalie
faida au uzuri wa ibara hizi na mapungufu au hasara zake.
FAIDA AU UZURI WA IBARA HIZI
( a )
Kwanza unapomwekea kinga rais hasa anapokuwa
madarakani ambao ndio wakati wa kutekeleza majukumu yake unakuwa umempa uhuru na umemwondolea woga katika kuamua na
kutoa maamuzi magumnu katika utekelezaji wa sera.
Rais anafanya mambo bila woga wala bila
kuhofia lolote jambo ambalo likitumiwa vyema laweza kutoa fursa kwa kushughulikia
mambo sugu yaliyoshindakana kama ufisadi hasa katika kuwashughulikia wale watu
wenye uwezo mkubwa wa kifedha au kimamlaka ambao hufanya matendo maovu kwa
kujiamini kutokana na kujijenga katika mitandao ya siasa ambayo wakati mwingine
hutishia hata mamlaka ya rais.
( b )
Pili unapoweka ugumu katika kumshtaki rais akiwa madarakani hakika unakuwa unajenga msingi wa amani na
utulivu. Kurahisisha kumshtaki rais kama
raia wa kawaida kunaweza kupelekea mashauri ya mara kwa mara dhidi yake kitu ambacho
kinaweza kuliyumbisha taifa kutokana na unyeti na ukubwa wa nafasi yenyewe.
0784482959 , 0714047241
KATIBA MPYA KUMALIZA USHINDI WA UBABAISHAJI UCHAGUZI MKUU
NA EMMANUEL
NDANU (WAKILI MAHAKAMA
KUU)
Katika uchambuzi wa leo wa
rasimu inayopendekezwa ili iwe katiba tumeona
ni vyema kuifanyia mapitio sura ya 8 ya
rasimu hii ambayo kwa ujumla
inazungumzia pamoja na mambo mengine
uchaguzi wa rais. Yako mambo mengi katika sura hii kumhusu rais au nafasi ya
rais lakini hayatazungumzwa yote
isipokuwa itaguswa Ibara ya 86 ( 6 )
ambayo inazungumza hivi
“ Mgombea wa nafasi ya madaraka ya Rais
atatangazwa kuwa
amechaguliwa
kuwa Rais iwapo atapata kura zaidi ya asilimia hamsini ya
kura
zote halali zilizopigwa kwa nafasi ya madaraka ya Rais.”
Kwa
kipindi cha takribani miaka kumi na tano iliyopita hili kwetu
halikuwako. Rais alikuwa akipata ushindi
hata kwa kumzidi mwenzake kura moja.
Ibara hii mpya katika rasimu inaleta
mfumo mpya wa kumpata rais. Ukifanya tathmini duniani utaona kuwa asilimia kubwa ya mataifa ambayo
hujinasibisha na mfumo wa demokrasia
hutumia mfumo huu wa asilimia
hamsini katika chaguzi zao.
Kwa walio wengi hapa kwetu hasa vijana
hususan miaka thelathini kushuka wanaweza kuona kitu hiki kama kigeni sana
katika nchi yetu. Ukweli ni kuwa utaratibu huu wa kumpata rais kwa mtindo wa asilimia hamsini si mgeni.
Itakumbukwa kuwa Katiba ya Jamhuri ya
Muungano ya 1977 ilikuwa na ibara ya
namna hii na chaguzi za kipindi hicho
zilifanyika katika utaratibu wa aliyezidi
asilimia hamsini ndio mshindi.
Ni mabadiliko ya 13 ya Katiba ya mwaka 2000
ndiyo yaliyoondoa utaratibu huu na kuweka utaratibu huu tulionao sasa ambapo mtu anaweza kutangazwa kuwa rais hata kwa kumzidi mwenzake kura moja. Hii ni
kusema kuwa mtindo huu sasa unakufa tunaanza mtindo wa asilimia ambao ndio
unaotumika kwa wingi hivi sasa duniani. Wapo wanaoona mtindo tuliokuwa nao ni mzuri na wapo
wanaoona mtindo mpya wa asilimia ni ndio mzuri zaidi. Inategemea na mtazamo
hasa kimaslahi.
Kihistoria chimbuko la utaratibu wa wingi wa kura kama tulionao na
wingi wa kura kwa asilimia ilikuwa ni katika jitihada za wanazuoni katika kutafsiri
maana ya neno KURA ZA WENGI (Majority Vote). Katika harakati hizo baadhi ya wanazuoni wakaja na
mawazo kuwa kura za wengi ni ile idadi kubwa
zaidi kuliko nyingine ikiwa na maana hata
kumzidi mtu kura moja tayari yule
aliyemzidi mwenzake kura moja anahesabika kuwa
ndiye aliyependwa na wengi zaidi kwakuwa amemzidi mwenzake kura moja.
Wanazuoni wengine wakakata wazo hili nao wakaja na wazo
kuwa wingi hauwezi kuhesabiwa hata kwa
kuzidiana kura moja isipokuwa maana ya wingi wa kura iwe ni wingi wa asilimia. Wakimaanisha kuwa ikiwa wtakaopiga kura ni alfu moja basi atakayepata zaidi ya nusu ya hizo ambazo ni zaidi ya mia tano huyo
ndiye atakayekuwa mshindi.Lakini ikiwa
mmoja amepata kura mia nne hamsini
na mwingine amepata miatatu kati ya alfu moja zilizopigwa basi hata huyu wa 450 hatahesabiwa kuwa ameshinda.
Yote ni mawazo tu ya wanazuoni ambayo ndio chimbuko la Ibara
hii. Mitazamo yote yaweza kuwa sahihi au hapana au mmoja waweza kuwa sahihi
zaidi kuliko mwingine. Zaidi ya hayo sisi pia
tuangalie faida na hasara za ibara iliyokaa katika mtindo huo.
FAIDA AU UZURI WA IBARA HII.
( a )
Uzuri wa kwanza wa kuhesabu ushindi kwa mtindo wa zaidi ya asilimia hamsini ni
kuwa taswira halisi ya mshindi kuwa ndio chaguo la wengi inajitokeza.
Chaguo la wengi linakuwa linakuwa chaguo
la wengi kweli. Hii ni kwakuwa mfumo huu
katika kuhesabu mshindi unazingatia idadi ya waliopiga kura na aliyevuka nusu
ya kura hizo.
Kwa mfano waliopiga kura ni laki moja hii ina maana ili mtu awe mshindi inabidi
apate zaidi ya elfu hamsini.Kimahesabu
wingi wa watu laki moja ni kweli kabisa unahesabiwa kuanzia zaidi ya nusu yake
ambao ni elfu hamsini. Hivyo anayepata
zaidi ya watu hao huyo kweli ndiye aliyependwa zaidi kwakuwa amependwa na zaidi
ya nusu.
Wakati ingekuwa katika mfumo ule tunaotumia
sasa ambao si wa asilimia hamsini kama
wapiga kura wangekuwa laki moja mgombea mmoja akapata kura mia tano na mwingine akapata mia tano na
mbili(502) na nyingine zikaenda kwa
wagombea wengine huyu wa mia tano na mbili angetangazwa mshindi bila kujali
zaidi ya kura elfu tisini na tano(95000)
zilizomkataa. Kwa hiyo utaona kuwa mtindo wa asilimia unajenga na kuleta taswira ya kweli katika
kanuni ya wingi wa kura (majority vote) katika kumpata mshindi.
( b )
Faida nyingine ya mshindi kwa wingi wa asilimia ni kuwa inaonesha kwa dhati kiwango cha kukubalika kwa mshindi. Mfano mfumo
tulionao sasa rais anaweza kuwa rais hata kwa kumzidi mwenzake kura moja tu.
Kwa hali ya kawaida ukimshinda mtu kwa kura moja picha inayokuja
ni kuwa pamoja na ushindi wa mgombea wako
wengi hawamkubali. Ina maana katika jamii iliyopiga kura mshindi na mpinzani
wake wanalingana katika kupendwa isipokuwa
tofauti yao ni mtu mmoja tu ambaye pengine naye amepatikana kwa kuwa
mshindi ana familia kubwa zaidi ya mshindwa.
Kimsingi hata mshindi wa kwanza na wa pili wakitofautiana
kura tano au hata kumi bado utaona kuwa
hata yule aliyemzidi mwenzake hakubaliki sana. Lakini kwa mtindo wa
asilimia hakuwezi kuwapo na tofauti ya
kura moja , mbili, kumi ishirini, thelathini na pengine hata mia. Utofauti wa
kura huwa ni mkubwa kiasi cha kujenga
taswira iliyo wazi kuwa mshindi anakubalika kwa
watu wengi zaidi kuliko mwenzake.
0784482959
0714047241
Subscribe to:
Comments (Atom)
