NA EMMANUEL
NDANU (WAKILI MAHAKAMA
KUU)
Katika uchambuzi wa leo wa
rasimu inayopendekezwa ili iwe katiba tumeona
ni vyema kuifanyia mapitio sura ya 8 ya
rasimu hii ambayo kwa ujumla
inazungumzia pamoja na mambo mengine
uchaguzi wa rais. Yako mambo mengi katika sura hii kumhusu rais au nafasi ya
rais lakini hayatazungumzwa yote
isipokuwa itaguswa Ibara ya 86 ( 6 )
ambayo inazungumza hivi
“ Mgombea wa nafasi ya madaraka ya Rais
atatangazwa kuwa
amechaguliwa
kuwa Rais iwapo atapata kura zaidi ya asilimia hamsini ya
kura
zote halali zilizopigwa kwa nafasi ya madaraka ya Rais.”
Kwa
kipindi cha takribani miaka kumi na tano iliyopita hili kwetu
halikuwako. Rais alikuwa akipata ushindi
hata kwa kumzidi mwenzake kura moja.
Ibara hii mpya katika rasimu inaleta
mfumo mpya wa kumpata rais. Ukifanya tathmini duniani utaona kuwa asilimia kubwa ya mataifa ambayo
hujinasibisha na mfumo wa demokrasia
hutumia mfumo huu wa asilimia
hamsini katika chaguzi zao.
Kwa walio wengi hapa kwetu hasa vijana
hususan miaka thelathini kushuka wanaweza kuona kitu hiki kama kigeni sana
katika nchi yetu. Ukweli ni kuwa utaratibu huu wa kumpata rais kwa mtindo wa asilimia hamsini si mgeni.
Itakumbukwa kuwa Katiba ya Jamhuri ya
Muungano ya 1977 ilikuwa na ibara ya
namna hii na chaguzi za kipindi hicho
zilifanyika katika utaratibu wa aliyezidi
asilimia hamsini ndio mshindi.
Ni mabadiliko ya 13 ya Katiba ya mwaka 2000
ndiyo yaliyoondoa utaratibu huu na kuweka utaratibu huu tulionao sasa ambapo mtu anaweza kutangazwa kuwa rais hata kwa kumzidi mwenzake kura moja. Hii ni
kusema kuwa mtindo huu sasa unakufa tunaanza mtindo wa asilimia ambao ndio
unaotumika kwa wingi hivi sasa duniani. Wapo wanaoona mtindo tuliokuwa nao ni mzuri na wapo
wanaoona mtindo mpya wa asilimia ni ndio mzuri zaidi. Inategemea na mtazamo
hasa kimaslahi.
Kihistoria chimbuko la utaratibu wa wingi wa kura kama tulionao na
wingi wa kura kwa asilimia ilikuwa ni katika jitihada za wanazuoni katika kutafsiri
maana ya neno KURA ZA WENGI (Majority Vote). Katika harakati hizo baadhi ya wanazuoni wakaja na
mawazo kuwa kura za wengi ni ile idadi kubwa
zaidi kuliko nyingine ikiwa na maana hata
kumzidi mtu kura moja tayari yule
aliyemzidi mwenzake kura moja anahesabika kuwa
ndiye aliyependwa na wengi zaidi kwakuwa amemzidi mwenzake kura moja.
Wanazuoni wengine wakakata wazo hili nao wakaja na wazo
kuwa wingi hauwezi kuhesabiwa hata kwa
kuzidiana kura moja isipokuwa maana ya wingi wa kura iwe ni wingi wa asilimia. Wakimaanisha kuwa ikiwa wtakaopiga kura ni alfu moja basi atakayepata zaidi ya nusu ya hizo ambazo ni zaidi ya mia tano huyo
ndiye atakayekuwa mshindi.Lakini ikiwa
mmoja amepata kura mia nne hamsini
na mwingine amepata miatatu kati ya alfu moja zilizopigwa basi hata huyu wa 450 hatahesabiwa kuwa ameshinda.
Yote ni mawazo tu ya wanazuoni ambayo ndio chimbuko la Ibara
hii. Mitazamo yote yaweza kuwa sahihi au hapana au mmoja waweza kuwa sahihi
zaidi kuliko mwingine. Zaidi ya hayo sisi pia
tuangalie faida na hasara za ibara iliyokaa katika mtindo huo.
FAIDA AU UZURI WA IBARA HII.
( a )
Uzuri wa kwanza wa kuhesabu ushindi kwa mtindo wa zaidi ya asilimia hamsini ni
kuwa taswira halisi ya mshindi kuwa ndio chaguo la wengi inajitokeza.
Chaguo la wengi linakuwa linakuwa chaguo
la wengi kweli. Hii ni kwakuwa mfumo huu
katika kuhesabu mshindi unazingatia idadi ya waliopiga kura na aliyevuka nusu
ya kura hizo.
Kwa mfano waliopiga kura ni laki moja hii ina maana ili mtu awe mshindi inabidi
apate zaidi ya elfu hamsini.Kimahesabu
wingi wa watu laki moja ni kweli kabisa unahesabiwa kuanzia zaidi ya nusu yake
ambao ni elfu hamsini. Hivyo anayepata
zaidi ya watu hao huyo kweli ndiye aliyependwa zaidi kwakuwa amependwa na zaidi
ya nusu.
Wakati ingekuwa katika mfumo ule tunaotumia
sasa ambao si wa asilimia hamsini kama
wapiga kura wangekuwa laki moja mgombea mmoja akapata kura mia tano na mwingine akapata mia tano na
mbili(502) na nyingine zikaenda kwa
wagombea wengine huyu wa mia tano na mbili angetangazwa mshindi bila kujali
zaidi ya kura elfu tisini na tano(95000)
zilizomkataa. Kwa hiyo utaona kuwa mtindo wa asilimia unajenga na kuleta taswira ya kweli katika
kanuni ya wingi wa kura (majority vote) katika kumpata mshindi.
( b )
Faida nyingine ya mshindi kwa wingi wa asilimia ni kuwa inaonesha kwa dhati kiwango cha kukubalika kwa mshindi. Mfano mfumo
tulionao sasa rais anaweza kuwa rais hata kwa kumzidi mwenzake kura moja tu.
Kwa hali ya kawaida ukimshinda mtu kwa kura moja picha inayokuja
ni kuwa pamoja na ushindi wa mgombea wako
wengi hawamkubali. Ina maana katika jamii iliyopiga kura mshindi na mpinzani
wake wanalingana katika kupendwa isipokuwa
tofauti yao ni mtu mmoja tu ambaye pengine naye amepatikana kwa kuwa
mshindi ana familia kubwa zaidi ya mshindwa.
Kimsingi hata mshindi wa kwanza na wa pili wakitofautiana
kura tano au hata kumi bado utaona kuwa
hata yule aliyemzidi mwenzake hakubaliki sana. Lakini kwa mtindo wa
asilimia hakuwezi kuwapo na tofauti ya
kura moja , mbili, kumi ishirini, thelathini na pengine hata mia. Utofauti wa
kura huwa ni mkubwa kiasi cha kujenga
taswira iliyo wazi kuwa mshindi anakubalika kwa
watu wengi zaidi kuliko mwenzake.
0784482959
0714047241
0 comments:
Post a Comment