NA MAWAKILI WETU.
Ni
ibara ya 70 katika rasimu iliyopitishwa
na Bunge Maalum la katiba bila watu
wajiitao UKAWA na ni Ibara ya 60 katika
rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba maarufu kama tume ya Warioba. Ni
ibara ya moto sana . Wengi wamekwisha
kufarikiana na wengine wamekwenda mbali
zaidi kiasi cha kutotoleana hata salamu. Sababu haswaa ya yote hayo ni Ibara
hiyo.Wanagombea nini na wanajengeana chuki kwa ajili gani. Ni kwa ajili ya
taifa na wanataifa ?, ni kwa ajili ya makundi yao wanayoita vyama vya siasa ?,
ni kwa ajili yao binafsi mmoja mmoja ?,
ni kwa ajili gani haswa. Siri wanayo wao. Nani wa kuaminiwa kati yao, na kwa
nini aaminike, kwa historia yake au kwa
analolisema leo jukwaani.
Ni kazi ngumu kutegua kitendawili
hiki. Anayetaka wepesi kidogo wa kutegua kitendawili hiki kanuni ni moja tu, nayo
ni kuwa mfuatiliaji wa karibu sana wa
mambo huku ukiepuka kupenda sana
kusimuliwa kuliko kufanya utafiti mwenyewe.
Leo
si kama jana, mambo yamerahisishwa taarifa zipo kila mahali zinamsubiri tu
wakuzipekua na kuzifanyia kazi. Mitandao ya kijamii na intanet kwa ujumla wake,mawasiliano
ya magazeti, redio na runinga vyote hivi vyaweza kukupa fursa ya kuwa na fikra huru .
Kwa kufanya hivyo utakuwa umejiweka mbali na kuburuzwa, mbali na ndio mzee,
ushabiki usio na tija na kuwa mbali na
virusi vingine vyote vyenye kuharibu akili. Epuka kughiribiwa hasa kipindi hiki
tunapoelekea kwenye kura ya maoni ya rasimu katiba .
Ibara
nilizotaja hapo juu ni kuhusu Muundo wa Muungano wa Serikali ya Tanzania katika
rasimu. Kawaida ya safu hii huwa
hatumshikii mtu akili wala hatufikirii
kwa niaba ya mwingine. Huwa inachukuliwa Ibara katika rasimu inatolewa maelezo na inaelezwa faida za na
hasara zake ili basi iwe fursa kwa
msomaji kutafakari mwenyewe na kujua upi mchele na ipi pumba.
SURA YA SABA IBARA 70. MUUNDO WA MUUNGANO.
Nukuu “Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania itakuwa na muundo wa Serikali
mbili
ambazo ni:
(a)
Serikali ya Jamhuri ya Muungano; na
(b)
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.” Mwisho
wa nukuu.
Ieleweke kuwa mamlaka ya nchi
hutekelezwa na kudhibitiwa na vyombo
vikuu vitatu. Serikali ni moja ya vyombo hivyo ambavyo vingine ni mahakama na
bunge. Vyombo hivi hufanya kazi kwa pamoja
huku kanuni ya udhibiti na urari
(checks and balance) ikiwa ndio msingi wa utekelezaji majukumu ya vyombo
hivi. Serikali zikiwa mbili maana yake ni kuwa na vyombo hivi vingine navyo
vitakuwa Viwili viwili. Serikali ya Mapinduzi bunge lake na mahakama zake,
serikali ya Tanzania bara kama inavyoitwa
nayo bunge lake na Mahakama yake. Kwa mfumo huu bunge na mahakama ya
Muungano ndio bunge na mahakama ya Tanzania bara wakati bunge na mahakama ya
Zanzibar si bunge na mahakama ya Muungano.
Hii ndio sura halisi ya Ibara hii kwa uwazi kabisa.
Kwa muonekano huu hakuna tofauti kati
ya rasimu na katiba hii ya sasa ambayo nayo inazungumzia kitu hikihiki.Mabadiliko
labda kama yatakuwa katika viunga,taasisi na namna ya madaraka katika utekelezaji
wa majukumu lakini kimuundo hakuna jipya .
Yumikini kila jambo lina faida na
hasara zake na ndio ada ya ukurasa huu kuainisha
baadhi ya faida na hasara ambazo zinazotokana na kuwapo kwa munndo wa aina hii.
Faida au hasara zinatokana na mambo mengi ikiwemo taasisi ambazo hupatikana
chini ya muundo, uongozi wake, mamlaka, uhusiano wa ndani na nje ya muungano,
uhusiano na vyombo vingine vya dola kama bunge na mahakama, mgongano wa masuala
ya sheria, maslahi ya wananchi ambao ndio chimbuko la mamlaka, uchumi wa nchi
husika na mengine mengi kama tutakavyoona
hapa chini.
FAIDA ZA MUUNDO
WA SERIKALI MBILI.
( a )
Ni ukweli ambao hauwezi kuwa na mpinzani kuwa serikali mbili zinapunguza gharama.
Lakini zinapunguza gharama ikiwa kuna pendelezo la kuwapo serikali tatu au nne.
Kukiwa na pendekezo la serikali
moja jibu haliwezi kuwa sawasawa. Upungufu
wake wa gharama unatokana na ukweli kuwa
ili Muungano ufanane na miungano mingine duniani ulitakiwa uwe na mamlaka tatu zilizo wazi , mamlaka huru ya
muungano , mamlaka huru ya Tanganyika na Mamlaka huru ya Zanzibar.
Badala yake
mamlaka zinakuwa mbili ya Tanganyika na Zanzibar
huku ya Tanganyika ikiingia katika ile mamlaka ya muungano na kuwa moja hivyo
kuua mamlaka moja na kubaki mbili. Mamlaka tatu maana yake ni kuwa kila mamlaka
na kiongozi wake mkuu awe rais au waziri mkuu, kiongozi mkuu msaidizi, itifaki
ya ulinzi inayojitegemea, vyombo vya usafiri vinavyojitegemea magari ya kutosha
, ndege, ofisi kubwa zenye hadhi na zinazojitegemea, watumishi wa kila idara na
kila kitu ambacho kinahitajika kwa sehemu kuitwa mamlaka ya dola. Hizo zote
tunaongelea fedha.
Hakuna maelezo hapo ni fedha tu .Kwa serikali mbili maana
yake ni kuwa vitu hivi vinagawanyika mara mbili tu na itifaki zote nilizotaja hapo
juu zinakuwa mara mbili badala ya tatu na hivyo kuweka wepesi katika gharama.
( b )
Serikali mbili zinaweka mbali uwezekano wa kuvunjika kwa muungano. Muungano
unapokuwa wa mkataba au serikali tatu
inasogeza karibu uwezekano wa kuuvunja muungano hasa kutoka kwa viongozi
ambao wanaweza kujitokeza wakiwa na fikra na sera zenye mrengo huo.
Muungano wa
serikali mbili unapunguza sana uhuru wa
washirika katika kuamua mambo yao hasa
upande wa Zanzibar kitu ambacho
kinalazimisha kuwapo kwa muungano. Kwa
mfano kwa muungano huu serikali ya Zanzibar haina uwezo wa kuamua kuwa sasa
tunajitoa katika muungano kutokana na namna
muungano wenyewe ulivyoundwa. Lakini kwa uhuru wa kimuundo wa serikali za mkataba au
serikali tatu jambo hili linawezekana kwa urahisi kwakuwa aina za muungano wa aina hiyo huwa inatoa
mwanya wa kufanya hivyo.Kila upande huwa unakuwa na uwezo wa kimustakabali
katika kuendelea na muungano au kutoendelea.
Huu wa serikali mbili hautoi mwanya
huo. Miaka ya sabini ilikuwa rahisi kulimaliza shirikisho la Afrika ya
Mashariki kwakuwa miungano ya shirikisho hutoa nafasi hizo. Shirikisho huwa ni makubaliano
tu kama yalivyo makubaliano mengine yote anayeona kabanwa anaachia kwakuwa katika makubaliano
hayo huwa lazima kuwe na vipengele vyanavyohusu namna ya kujitoa. Hivyo niseme
tu kuwa muungano wa serikali mbili
hivihivi zilivyo bila kugusia lolote kuhusu
upande mmoja kukaliwa au kutokaliwa unatoa nafasi ya lazima katika
kuwepo kwake. Unalazimisha maisha yake.
( c )
Pia kwa kuweka serikali mbili Ibara hii inawaweka karibu zaidi watu wa Zanzibar
na Tanganyika. Ibara inawaweka karibu zaidi kwa kulinganisha na serikaki tatu
au mkataba na si kwa kulinganisha na serikali moja ambayo ndiyo ingewaweka
karibu zaidi kuliko zote. Panapokuwa na serikali tatu au mkataba wazo linalojengeka ni kuwa mnashirikiana tu kama ambavyo mnaweza
kushirikiana na Kenya na Uganda au kama ambavyo mnaweza kushirikiana na
Marekani au nchi nyingine yoyote. Ile hali ya kuwa hamshirikiani isipokuwa nyie ni ndugu na
mnayofanya ni kwa ajili ya udugu taratibu inaanza kutoweka.
Mnakuwa kama majirani wengine wowote na lile
fungamano(commitment) la kuwa nyie ni ndugu
linatafunwa mpaka kufikia kuwa washirika wa kawaida kabisa. Ushirika ni mwepesi
na unapunguza umakini (seriuosness) katika kujaliana (careness). Muundo wa
serikali mbili unaondoa hali ya ushirika
wa kawaida.
0784492959
0714047241
0 comments:
Post a Comment