NA
JACKLINE MAJURE (WAKILI
MAHAKAMA KUU)
Ibara ya 93 katika rasimu
inayopendekezwa ili iwe katiba inasema
hivi 93.-(1)”
Wakati Rais akiwa madarakani, hatashtakiwa wala mtu yeyote
hataendesha
mashtaka ya aina yoyote dhidi yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la
jinai”.
Ni
aina ya ibara ambayo inatoa kinga kwa mtu atakayekuwa ameshika madaraka ya rais kutoshitakiwa. Katika ibara hii
kuna mambo matatu ya kuzingatia, Kwanza
kabisa ibara hii inazungumzia wakati
rais anapokuwa madarakani yaani wakati yuko
ikulu ndo asifunguliwe mashtaka, lakini
pili mashtaka yenyewe ambayo hapaswi kufunguliwa ni yale Mashtaka ya kijinai tu ambayo ni kama kuua,
kubaka, kulawiti,kupiga, kuiba, rushwa, uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya
ofisi n.k. Tatu sehemu anapozuiwa kushtakiwa ni mahakamani wala si bungeni.
Kwa
kawaida viongozi wakuu hasa marais wakati mwingine hushtakiwa mahakamani au
bungeni lakini kwa hapa imezuiwa
kumshtaki makahamani wala si bungeni.Kwahiyo ibara hii ndogo ya ( 1 ) imeundwa
na mambo hayo matatu.
Aidha Ibara hiyohiyo Ibara
ndogo ya (2) inasema hivi
“Wakati Rais ameshika madaraka kwa mujibu wa Katiba hii,haitaruhusiwa
kufungua mahakamani shauri la madai kuhusu jambo lolote alilolitenda au
alilokosa kulitenda yeye binafsi kama Rais ama kabla au baada ya kushika
madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku thelathini kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais atapewa au
ametumiwa taarifa ya madai kwa maandishi
kwa kufuata utaratibu utakaowekwa kwa mujibu wa sheria, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo kuhusu chanzo cha
shauri hilo, kiini cha madai yenyewe,
jina lake na anwani ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai”
Ibara
hii inatoa nafasi kwa rais aliye madarakani kushtakiwa kwa makosa ya madai. Ile
ibara ya kwanza ya juu inakataza kumshtraki kwa makosa ya jinai wakati akiwa
madarakani. Hii sasa inaruhusu kushtakiwa hata akiwa madarakani lakini kwa
makosa ya madai tu. Makosa ya madai ni kama kugombea mashamba,viwanja au
nyumba, kukopeshana vitu vya thamani kama fedha na kushindwa kulipa, kudai
fidia baada ya kutukanwa au kudhalilishwa,kuvunja mkataba kama mikataba ya
mauziano ya vitu kama magari n.k. Hayo ndio makosa ya madai ambayo rais hata akiwa madarakani
waweza kumshtaki nayo.
Aidha jambo jingine la
tofauti limejitokeza katka ibara
hiyohiyo ya 93 ibara ndogo ya (3) ambayo inasema hivi “ Isipokuwa kama ataacha kushika
madaraka ya Rais kutokana na kuondolewa madarakani na Bunge, haitakuwa halali
kwa mtu kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la madai dhidi
ya mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo
kutokana na jambo
alilofanya
wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais”.
Kwanza tuliona hairuhisiwi kumshtaki
rais kwa kosa lolote la jinai pale anapokua madarakani, pili tumeona
inaruhusiwa kumshtaki rais kwa kosa la madai hata akiwa madarakani na sasa
tunaona kuwa itakapotokea bunge limemwondoa rais madarakani basi hakuna ruhusa mtu au chombo chochote kumshtaki rais kwa kosa
lolote liwe la jinai au la madai alilofanya akiwa madarakani.
Sura ya jumla ya ibara hizi zote kwa pamoja ni
kuwa kwanza rais hashtakiwi kwa kosa lolote la jinai iwe pale anapokuwa madarakani au hata baada
ya kutoka. Makosa yote ya jinai aliyoyafanya wakati akiwa ikulu hayaguswi
kabisa. Pili ni kuwa anayetaka kumshtaki
rais kwa kosa la madai amshtaki akiwa bado yuko madarakani lakini akishatoka
basi huwezi tena kumshtaki hasa kama ametoka kwa kuondolewa na bunge. Tuangalie
faida au uzuri wa ibara hizi na mapungufu au hasara zake.
FAIDA AU UZURI WA IBARA HIZI
( a )
Kwanza unapomwekea kinga rais hasa anapokuwa
madarakani ambao ndio wakati wa kutekeleza majukumu yake unakuwa umempa uhuru na umemwondolea woga katika kuamua na
kutoa maamuzi magumnu katika utekelezaji wa sera.
Rais anafanya mambo bila woga wala bila
kuhofia lolote jambo ambalo likitumiwa vyema laweza kutoa fursa kwa kushughulikia
mambo sugu yaliyoshindakana kama ufisadi hasa katika kuwashughulikia wale watu
wenye uwezo mkubwa wa kifedha au kimamlaka ambao hufanya matendo maovu kwa
kujiamini kutokana na kujijenga katika mitandao ya siasa ambayo wakati mwingine
hutishia hata mamlaka ya rais.
( b )
Pili unapoweka ugumu katika kumshtaki rais akiwa madarakani hakika unakuwa unajenga msingi wa amani na
utulivu. Kurahisisha kumshtaki rais kama
raia wa kawaida kunaweza kupelekea mashauri ya mara kwa mara dhidi yake kitu ambacho
kinaweza kuliyumbisha taifa kutokana na unyeti na ukubwa wa nafasi yenyewe.
0784482959 , 0714047241
0 comments:
Post a Comment