
NA JACKLINE MAJURE ( WAKILI MAHAKAMA
KUU)
Ibara ya 216.-(1) katika rasimu inayopendekezwa ili iwe
katiba kama itapita inasema kama
ifuatavyo “Bila kuathiri masharti ya Ibara ya 88
na Ibara ya 140, mtu atakuwa na haki ya kuwa mgombea huru katika uchaguzi
unaosimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi”.
Ni kwa maana hii kuwa ule
utaratibu wetu wa kuwa
kila mgombea ubunge au urais au udiwani
ni lazima awe ametokana na chama chochote cha siasa
utakuwa umekufa. Haufi kwa maana
kuwa vyama sasa vimepigwa marufuku
hapana, isipokuwa si lazima kupitia chama cha siasa ili mtu awe
kiongozi kwa njia ya
kuchaguliwa.
Mgombea huru atakuwa ni mgombea ambaye hatokani na chama chochote
cha siasa na ataweza kugombea
ubunge udiwani na hata mamlaka
makubwa ya urais ataruhusiwa kugombea. Pia ugombea huru umeainishwa kama
sifa maalum kwa mtu ambaye havutiwi na siasa za vyama katika kugombea ubunge.
Ibara ya 140( 1 ) inasema hivi
“Bila kuathiri masharti yaliyomo
katika Ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa
mbunge endapo:
|
(a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano
aliyetimiza umri wa miaka ishirini na moja wakati wa kugombea;
|
(b) anajua kusoma na
kuandika lugha ya Kiswahili au Kingereza; na
|
(c) ni mwanachama
aliyependekezwa na chama cha siasa au mgombea HURU.
|
Baada ya kutimiza sifa zilizoainishwa ambazo ni kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano, kujua kusoma
na kuandika kati ya lugha ya
Kiswahili ama kiingereza lakini basi mtu asiye
na chama chochote cha siasa anaweza
kuomba ridhaa ya wananchi ili awe mwakilishi wao bungeni. Kwa mamlaka ya rais Ibara ya 88 baada ya sifa nyingine kutimia imetoa ruksa
kwa mgombea huru kuwania mamlaka
hayo kama ifuatavyo ;
88.-(1)
Mtu atakuwa na sifa ya kuchaguliwa kushika nafasi ya madaraka ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano ikiwa:
|
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya
Muungano
|
(f) ni mwanachama na
mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa au mgombea HURU.
|
Aidha katika yote hayo ibara ya 143.-(1) inaibua kitu kingine
kuhusu mgombea binafsi kama inavyonukuliwa hapa, “Mbunge atakoma kuwa Mbunge ikiwa
litatokea lolote kati ya mambo yafuatayo:
(h) Mbunge aliyetokana na mgombea huru,
atajiunga na chama chochote cha siasa”
|
Kawaida tumezoea kusikia diwani,mbunge au rais akiacha chama
chake cha siasa anapoteza hata mamlaka yake. Ni kwasababu hii tumeshashuhudia
mara nyingi baadhi ya viongozi wa siasa wakikimbilia
mahakamani kulinda nyadhifa zao baada ya
kutishiwa uanachama wao kwenye
vyama vyao vya siasa. Kwahiyo kama zamani kuacha uanachama ilikuwa ndio upoteze mamlaka
sasa hata kuingia uanachama nako
kutampelekea mwanasiasa kupoteza mamlaka. Kwa ufupi tuangalie faida na hasara za mgombea huru katika
ibara hizi.
FAIDA ZA MGOMBEA
HURU
( a ) Kwanza imepanua wigo wa
demokrasia kwa kuwashrikisha watu wengi zaidi katika kuomba ridhaa ya nyadhifa mbambnali. Wako watu wengi ambao walikuwa
wakitaka nyadhifa za siasa lakini
hawapendi siasa za vyama. Kwa
ibara hii ni kusema kuwa hawa nao
wameingizwa katika kinyanganyiro na
hivyo sasa ushiriki utaongezeka.
( b ) Mgombea binafsi atongeza ushindani hasa majimboni. Wako watu ambao walikuwa na
uwezo mzuri wa kuwa viongozi na wanakubalika sana kwa
wananchi lakini wanaenguliwa katika kinyanganyiro kutokana na hila ndani ya vyama. Kwa kuwapo
mgombea huru itakuwa
chama kikimuengua mtu anayekubalika
kwa wananchi basi kijiandae kupambana naye kwa ushindani mkubwa katika uchaguzi.
( c )Itapelekea kupatikana viongozi wenye uwezo kiuongozi na si kiongozi mwenye uwezo kimtandao wa siasa. Mara nyingi viongozi wanaopatikana
kupitia vyama vya siasa ni wale wenye
mitandao madhubuti katika vyama hivyo
na si wale wenye uwezo kuiongozi.
Hili wala sio siri viongozi wetu wengi wamepatikana kwa nguvu za mitandao hasa
mitandao fedha na si uwezo binafsi
kiuongozi
0784482959, 0714047241
0 comments:
Post a Comment