Sura ya pili, sehemu ya pili ibara ya 12( 1 ) ya rasimu inayopendekezwa
kuwa katiba inasema kuwa
“Lengo
la Katiba hii kisiasa ni kudumisha demokrasia”.
Rasimu inayasema haya ikiwa katika
harakati za kuelezea malengo ya taifa ya kisiasa.Kimsingi katika rasimu yako malengo ya taifa ya kijamii(
social vision), malengo ya taifa ya kiutamaduni( cultural vision), malengo ya
taifa ya kiuchumi( economic vision) na malengo ya taifa kisiasa( political vision) ambayo ndio tunayaangalia
sasa.
Ukisikia malengo ya taifa kisiasa au
kijamii maana yake ni mwelekeo wa
taifa kisiasa au kijamii. Mwelekeo maana
yake ni kuwa kila kitakachokuwa
kinafanyika nchini lazima kiwe kinafanana na kile kilichosemwa katika katiba. Taasisi zote za dola na za kiraia lazima
zihakikishe shughuli zake zote zinafanana na lengo la kisiasa katika katiba. Na
kwakuwa lengo la kisiasa ni demokrasia basi
kila taasisi ya kidola au binafsi lazima ihakikishe shughuli zake zinafanana na demokrasia.
Hii maana yake ni kuwa demokrasia itakuwa ndio kioo. Taasisi au mtu
binafsi atakuwa anatakiwa kujitazama na
kuona kama anafanana na demokrasia
iliyosemwa katika katiba ambapo akiona anafanana basi hiyo shughuli anayoifanya ni halali kwakuwa ina baraka za katiba na akiona haifanani
basi shughuli hiyo ni haramu na yuko katika hatari ya kuchukuliwa hatua za
kisheria kwa kukiuka katiba.
Ni sawa na kusema kuwa demokrasia kiwe ndio kiigizo chetu, iwe
ndio mfano wetu.Hiyo ndio maana ya demokrasia kuwa lengo la taifa kisiasa. Kwa
maneno kama haya utaona ni kwa namna gani demokrasia imetukuzwa na kupewa hashima ya pekee kiasi cha
kupendekezwa kuwa kiigizo kwa Watanzania zaidi ya milioni 45.
Hii demokrasia nini mpaka ipate heshima kubwa
kiasi cha kuwa lengo kuu,kiigizo kikuu, mwelekeo mkuu,
na mfano mkuu wa watu zaidi ya milioni
45 kitaifa.
DEMOKRASIA NININI.
Ziko tafsiri nyingi na maarufu za
demokrasia ambazo wengi wetu tunazijua.
Sitaeleza tafsiri yoyote katika hizo isipokuwa nitaeleza wazo la jumla kuhusu hiki
kitu kinachoitwa demokrasia ambacho
katiba yetu mpya imetuelekeza
kukisujudia.
Ukitaka kumweleza mtu wa kawaida kabisa maana ya demokrasia mwambie hivi, demokrasia ni
haya maisha unayoyaona sasa,watu wanavaa wanavyotaka, watu wanatembea kulala na
kula wanavyotaka, mtu anaamua awanie uongozi au hapana, mtu anaamua nani awe kiongozi wake na nani asiwe, mtu
anaoa au kuolewa na anayemtaka, mtu anamkosoa
anayemtaka awe kiongozi wake mkuu au
mdogo, mtu anazungumza anavyotaka , mtu anaruhusiwa kuishi popote na bila kubughudhiwa,
yaani kwa ufupi kila uhuru wa kutenda
jambo unaouona hiyo ndio demokrasia.Mtu atakuelewa vyema.
DEMOKRASIA NDIO UBEPARI
Matendo ya kufanya mambo kwa uhuru
yameanza mamilioni ya miaka iliyopita isipokuwa hayakuwa yakiitwa demokrasia.
Walioanzisha demokrasia walichukua baadhi ya
matendo huru wakayaingiza katika huo mfumo wao wakayaita demokrasia.
Lakini
matendo kama uhuru wa kuongea(maoni), kutembea , kuvaa n.k yalikuwapo kabla ya
kitu kiitwacho demokrasia na umri wa matendo haya waweza kuwa sawa na umri wa
mwanadamu duniani.Aidha demokrasia hii tuliyonayo leo imeanza karne ya 15 kipindi cha hatua ya kwanza ya ubepari(
mechantalism) na imekua mpaka hatua ya sasa ya ubepari ambayo huitwa ubepari uliokomaa(monopoly
capitalism).
Kimsingi demokrasia ndio sera kuu ya
ubepari na neno demokrasia limeanzishwa na mabepari. Kwa maana hiyo tunapoamrishwa na katiba kuwa
demokrasia iwe ndio kiigizo, chetu, na
mfano wetu tunaambiwa kuwa kiigizo, na mfano wetu uwe ubepari.Ubepari(Capitalism)
ndio unaomiliki kitu kiitwacho demokrasia hili wala halina shaka. Kwa ibara hii
maana yake ni kuwa mwelekeo wa nchi hii ni ubepari na nchi hii sasa ni ya
kibepari rasmi.
MATATIZO YA KUFUATA UBEPARI.
( a )
Ielewewke kwamba ubepari ni mali ya watu na bila shaka walioanzisha na kumiliki
mali hiyo wanayo malengo yao. Miaka ya nyuma kiongozi wa ubepari alikuwa Wingereza
na sasa kiongozi wa ubepari ni Marekani. Wakati Wingereza akiongoza ubepari
alitumia nafasi hiyo hasa kwa mgongo wa
demokrasia kuingia Afrika na kuitawala
Afrika akishirikiana na wenzake wa ulaya.
Walijifanya wamekuja na mfumo mpya wa uongozi ambao ungeweza kumaliza
matatizo na shida za watu huku wakijua
na kuamini kuwa mfumo huo wenyeji wasingeweza
kumudu misingi yake kutokana na elimu na weledi mdogo na hivyo kujikuta
wameangukia mikononi mwa wageni.Kwa ufupi tuliweza kutawaliwa kwa urahisi
kutokana na kuzidiwa na mbinu za hiki kinachoitwa demokrasia.
( b )
Leo Amerika ameweza kuwa na amri juu ya dunia kupitia hiki kitu kinachoitwa
demokrasia. Mila na tamaduni za asili ambazo zimezaa maadili mema na mwenendo
mwema katika jamii zetu kwa muda mrefu zimekufa
na zimeuliwa na hiki kiumbe demokrasia.Tunashuhudia mavazi ya
hovyo,vitendo vya ukahaba, ushoga,
heshima kutoweka kwa mkubwa na mdogo, usagaji, na ghasia nyingine nyingi kwa
mgongo wa huyu demokrasia.
( c )
Wameandaa vitu wakaviita misingi mikuu ya demokrasia huku wakiamini kuwa hakuna
yeyote atakayeweza kufaidika na vitu
hivyo isipokuwa wao. Mfano, moja ya msingi wa demokrasia ni kuwa na uhuru
katika uchumi au uchumi huria. Katika uchumi huru ndimo penye uwekezaji kimataifa.
Ndani ya uwekezaji wa kimataifa
ndimo ilimo fursa ya wao kuja kuogelea
katika rasilimali zetu. Walijua uhuru katika uwekezaji wa kimataifa hakuna mwafrika atayekuwa
na uwezo wa kuwekeza kitu cha maana kwao. Isipokuwa wao ndio wataokuja
kuvinjari ndani ya migodi yetu,maziwa yetu, bahari, mafuta, gesi, na kila kitu.Demokrasia
ni mali ya watu na wenye nayo wanayo malengo
yao.
Tunatoa uhauri kuwa pamoja na maono
mazuri ya katibas mpya katika kukuza na kuimarisha
demokrasia tunapenda kusema
kama alivyosema aliyekuwa
rais wa Libya marehemu Kanali Muammar Gaddafi kuwa demokrasia nzuri
ni ile isiyoharibu mila desturi za wenyeji pia ni
ile isiyotumka kuingiza fikra za
kinyonyaji.
0784482959
0714047241
0 comments:
Post a Comment